Sunday, November 18, 2012

SERENGETI BOYS YAITOA NISHAI CONGO BRAZZAVILLE KWA KUIFUNGA 1-0


Wachezaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ya Serengeti Boys wakishangilia bao lililofungwa na Mudathiri Yahaya Abbas wakati timu hiyo ilipopambana na Congo Brazzaville katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Afrika kwa vijana wenye umri huo, zitakazofanyika mwakani nchini Morocco. Serengeti Boys imeshinda 1-0. (Picha zote na Habari Mseto Blog)


Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Jacob Michelsen na msaidizi wake Jamhuru Kihwelo wakipongezana baada ya mchezo kumalizika.

  Mshambuliaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ya Serengeti Boys, Hussein Twaha akiwatoka mabeki wa timu ya Congo Brazzaville katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za Afrika kwa vijana wenye umri huo zitakazofanyika mwakani nchini Morocco. Mchezo huo ulifanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Serengeti Boys imeshinda 1-0.

Mshambuliaji wa timu ya Srengeti Boys, Faridi Mussa (katikati) akiwania mpira huku beki wa Cpngo Brazzaville, Tmouele Ngampio akijaribu kumzuia. Kulia ni Golipika wa Congo Brazzaville, Ombandza Mpea akijaribu kuokoa hatario langoni mwake.


Mshambuliaji wa Serengeti Boys, Tumain Baraka akichuana na beki wa Congo Brazzaville, Okombi Francis


Heka heka katika lango la Congo Brazzaville


Wachezaji wa Serengeti Boys, Hussein Twaha (shoto), Joseph Lubasha na Selemani Hamis Bofu wakibadilioshana mawazo wakati wakitoka mapumziko

Selemani Hamis Bofu akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Congo Brazzaville, Tmouele Ngampio
PICHA ZOTE KWA HISANI YA:www.francisdande.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

only comments that are benefial for this blog is allowed