Katibu mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye
Shirikisho la soka
nchini Tanzania (TFF) limethibitisha kwa Shirikisho la Vyama vya Mpira
wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), kuwa timu ya taifa ya
wanawake ya Tanzania itashiriki michuano ya kwanza ya Kombe la Chalenji
kwa wanawake itakayofanyika kuanzia Septemba 11, 2016 hadi Septemba 20,
2016 kwa kushirikisha nchi saba wanachama wa shirikisho hilo.
Kwa
mujibu wa CECAFA, michuano hiyo itafanyika jijini Jinja na Tanzania
ambayo inaongoza kwa ubora wa viwango vya Mpira wa Miguu kwa nchi za
Afrika Mashariki imepangwa kundi B ikiwa pamoja na timu za Rwanda na
Ethiopia wakati kundi A litakuwa na timu za Kenya, Burundi, Zanzibar
pamoja na mwenyeji Uganda.
Tanzania itafungua michezo hiyo kwa kucheza na Rwanda Septemba 12, 2016 kabla ya kucheza na Ethiopia Septemba 16, 2016.