MAOFISA WA FIFA WATUA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO
OFISA Maendeleo wa Kusini mwa Afrika wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Ashford Mamelodi amewasili leo kwa ajili ya kufuatilia shughuli za maendeleo ya mpira wa miguu nchini.
Mamelodi, ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa shughuli za maendeleo nchini Tanzania tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, pia amekuja kumtambulisha msaidizi wake, Patrick Onyango aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo hivi karibuni.
Wakiwa nchini, wawili hao wanatarajiwa kupata taarifa ya maendeleo ya mradi wa kuweka nyasi bandia kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza, baada ya FIFA kuipa Tanzania mradi wa nne (GOAL Project 4) wa kuweka miundombinu kusaidia maendeleo ya mpira wa miguu.
Mamelodi, ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa shughuli za maendeleo nchini Tanzania tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, pia amekuja kumtambulisha msaidizi wake, Patrick Onyango aliyeteuliwa kushika nafasi hiyo hivi karibuni.
Wakiwa nchini, wawili hao wanatarajiwa kupata taarifa ya maendeleo ya mradi wa kuweka nyasi bandia kwenye Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza, baada ya FIFA kuipa Tanzania mradi wa nne (GOAL Project 4) wa kuweka miundombinu kusaidia maendeleo ya mpira wa miguu.
Mwanza ilipata mradi huo baada ya Halmashauri ya Jiji hilo kukubali masharti ya mradi huo ya kulipia nakisi ya fedha zinazolipwa na FIFA, ambazo ni sh. milioni 700. Mradi huo wa kuweka nyasi bandia Nyamagana utagharimu sh. milioni 900, hivyo nakisi y ash. milioni 200 italipiwa na Jiji la Mwanza.
Pia Mamelodi na Onyango watapata taarifa ya maendeleo ya Uwanja wa Gombani uliowekwa nyasi za bandia kwa msaada wa FIFA katika mradi wa GOAL Project 3; na pia kupata mikakati ya maendeleo ya TFF kwa mwaka 2013, ikiwa ni pamoja na kozi na semina mbalimbali zitakazofanyika nchini mwaka huu.
Mamelodi na Onyango pia watapata taarifa ya maendeleo ya uboreshaji wa mashindano ya Copa Coca-Cola baada ya FIFA kuingia rasmi kwenye mashindano hayo mwaka jana kwa kuendesha kozi kwa walimu wa timu za kombaini ya mikoa na waamuzi.
Kwa sasa mashindano hayo yanashirikisha vijana wenye umri chini ya miaka 17, lakini FIFA inataka yahusishe umri mdogo zaidi ili kuendeleza soka ya vijana na kushirikisha kikamilifu shule. Maofisa hao wataondoka nchini Jumatatu asubuhi.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
| YANGA NA AZAM ZAPIGANIA USUKANI WA LIGI |
LIGI
Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho
(Februari 23 mwaka huu) kwa mechi tatu, lakini macho na masikio ya
washabiki wa mpira wa miguu yatakuwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Uwanja
huo wa kisasa utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Yanga na makamu bingwa
Azam. Ingawa Azam imecheza mechi moja zaidi, lakini timu hizo
zinatofautishwa kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa kwenye
msimamo wa ligi huku kila moja ikiwa na pointi 36.
Pia
vinara wa ufungaji kwenye ligi kwa sasa wanatoka katika timu hizo
mbili. Kipre Tchetche aliyepachika mabao tisa hadi sasa ndiye
anayeongoza akifuatiwa na Didier Kavumbagu wa Yanga mwenye mabao manane.
Iwapo
timu yoyote itafanikiwa kuondoka na pointi tatu katika mechi hiyo
itakayochezeshwa na mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar es Salaam, kasi ya
mbio za kuwania ubingwa itaongezeka. Waamuzi wasaidizi watakuwa Hamis
Chang’walu wa Dar es Salaam na John Kanyenye kutoka Mbeya wakati mezani
atakuwepo Oden Mbaga.
Mechi
nyingine za kesho ni Mgambo Shooting dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa
Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakati Tanzania Prisons watakuwa wenyeji wa
Polisi Dodoma kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Jumapili
(Februari 24 mwaka huu), Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam utakuwa katika
hekaheka nyingine kwa Simba chini ya Mfaransa Patrick Liewig kuikabili
Mtibwa Sugar inayonolewa na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky
Maxime.
|

No comments:
Post a Comment
only comments that are benefial for this blog is allowed