Wednesday, July 15, 2015

Timu 6 kukata utepe,CECAFA


Ratiba ya mechi ya mechi za ufunguzi katika michuano ya Kombe la Kagame CECAFA imekwisha kufahamika ambapo jumamosi hii APR ya Rwanda itakwana na Al Shandy ya Sudan majira ya saa nane mchana kwa saa za afrika mashariki.

Mechi ya pili itakuwa kati yaYanga ya Tanzania na Gor Mahia ya Kenya mchezo utakao chezwa saa saa 10 za jioni kwa saa za Afrika mashariki. Muda huo huo KMKM kutoka visiwa vya Karafuu Zanzibar itakuwa na mtihani mkali pia dhidi ya Telecom ya Djibout.

Katika historia ya michuano hiyo,Simba ya Tanzania ndiyo inaongoza kwa kutwaa ubingwa mara nyingi,kwani ni mara sita hadi sasa ikifuatiwa na Yanga huku Gr Mahia ikiwa imetwaa mara tano na APR ya Rwanda mara tatu.

No comments:

Post a Comment

only comments that are benefial for this blog is allowed